Ay-Ayo, Trone
Mmh
Ni utoto tu, ila mie kwako sipindui
Ndio maana usiku nikinuna, najichekesha asubuhi
Ni ujinga tu, ila mie kwako fala
Ndio maana usipo pokea simu, siwezagi lala
Mm, umenifunza tofauti ya kupenda na kupendana
Na kuongea sio sauti hata macho husemezana
Na mapenzi yanataka, 'imara, kuaminiana
Nami kwako sina shaka, 'ewawa, utachofanya
Na hivi vi inzi, vya kuzengea wizi
Vikija anga hizi, visikunyime amani
Lala usingizi, upepo barizi
Mie mambo ya uzinzi, 'aku vya kazi gani, baby?
Hapo hapo ilipo mbao (gongelea na msumari)
Oh, penzi letu tuboreshe (gongelea na msumari)
Ezeka na bati, honey (gongelea na msumari)
Mvua ya chuki isipenyeshwe (gongelea na msumari)
Mm, mm-m
Oh, njiwa nenda, njiwa, 'njiwa peleka salamu (peleka salamu)
Naivasha, Kivule, 'Mombasa zifike Lamu
Njiwa nenda, njiwa, 'njiwa peleka salamu
Ziende mpaka kwa yule, 'lonitesa mwanaharamu
Si alisema mimi, sitopata wa thamani
Asa hii ni nini? Umuulize huyu nani
Wamebaki kutabiri si punde tutaachana
Wambie sio kwa penzi hili, mbona wataroga sana
Na hivi vi inzi, vya kuzengea wizi
Vikija anga hizi, visikunyime amani
Lala usingizi wewe, upepo barizi
Mie mambo ya uzinzi, 'aku vya kazi gani, baby?
Hapo hapo ilipo mbao (gongelea na msumari)
Oh, penzi letu tuboreshe, darling (gongelea na msumari)
Ezeka na bati, honey, oh (gongelea na msumari)
Mvua ya chuki isipenyeshwe (gongelea na msumari)
Mm
Wasafi